UKEKETAJI.....hauna faida mbali maafa kibao katika Afya ya wanawake , Ungana nami kukomesha ukeketaji..elimisha jamii madhara ya kiafya na vifo vinavyotokana na UKEKETAJI!
http://twitter.com/Mashua
http://www.facebook.com/pages/Mashua-Against-FGM/225406701415?ref=ts
Ukeketaji unakwenda kinyume cha uumbaji wa Mungu. Mungu akamuumba mtu kwa
mfano wake.
Ukeketaji unakiuka haki za mwanamke na msichana kama zinavyoelezwa katika mkataba
wa kimataifa dhidi ya ubaguzi wa aina zote kwa wanawake wa mwaka 1979 (CEDAW)
Mkataba wa kimataifa juu ya haki za mtoto wa 1989 na tamko la kiafrika juu ya haki na
ustawi wa mtoto. Ukeketaji unasababisha maumivu ya kudumu ulemavu na hata vifo.
Kipekee ukatili huu unavunja haki, utu na heshima ya mwanamke na mtoto.
c. Ukeketaji una madhara mengi kwa wanawake na wasichana na watoto wanaotendewa
jambo hilo. Wanawake waliokeketwa wanaathirika kiafya, kisaikolojia, kijamii na
kiuchumi na mengineyo kwa mfano:
- Athari za kiafya ni pamoja na:
i. Maumivu makali wakati wa kukeketwa
ii. Kuvuja damu nyingi wakati wa kukeketwa na wakati wa kujifungua
iii. Kupata makovu ambayo huchanika vibaya wakati wa kujifungua Kuvimba maeneo ya
siri kama tunavyoona wengine wanaovimba masikio wakati wanapotoga masikio yao.
iv. Kupata maambukizi ya magonjwa hasa VVU wakati wa kukeketwa na mengineyo.
Athari za kijamii baadhi ni kama zifuatazo:
i. Tendo la ndoa kukosa msisimuko au raha kwa mwanamke na kuwa kero
ii. Kukosa watoto ukeketaji unapokosewa.
Athari za kisaikolojia ni pamoja na:
i. Mwanamke kuwa na maumivu ya kudumu
ii. Kuchukia tendo la ndoa
iii. Kujisikia kutotoshelezwa wakati wa tendo la ndoa.
Madhara au athari hizi zinakuwa jinamizi linalomfuata mwanamke maisha yake yote.
Balozi Lucy Mashua ,
Balozi wa kukabiliana na ukeketaji duniani.
Msaidizi wa wakimbizi hapa Marekani
Mwenye kiti wa kamati inoyopinga ukeketaji duniani.
Kuongeza raha ya mwanamume katika tendo la ndoa
Kuondoa ugumba, magonjwa ya kizazi nuksi na mikosi, n.k.
Kumtawala mwanamke (mfumo dume) na mengine yafanayo na hayo.
je huu ni ungwana?
lmashua 2 years ago
Mila
na imani zinazohusiana na ukeketaji zina madhumuni au makusudi fulani
yanayotakiwa kufikiwa na jamii husika. Kwa mfano ukeketaji una
madhumuni yafuatayo:-
Kumwondoa msichana kutoka rika la utoto na kuingia utu uzima.
Kumzuia msichana asiwe na tamaa ya kujamiiana na wanaume ovyo
ovyo.
Mahari- wazazi wenye watoto waliokeketwa wanayo nafasi kubwa ya kupata mahari kubwa kwa ajili ya watoto wao.
lmashua 2 years ago
Tukilichunguza tatizo hili kwa muhtasari tunaona kwamba tabia ya ukeketaji
imejengeka katika mila na imani za watu kufuatana na mazingira yao.
lmashua 2 years ago
Great. No defense can be made for preserving a cultural practice that damages womens' health and interferes with their sexuality. Good Luck!
siasabora 2 years ago
@siasabora Shukrani Siasa bora naumenitupa mno;)
lmashua 2 years ago