Mwenyezi Mungu amesema kwenye Quran, surat Al Imran, aya ya 19, Akimaanisha: Dini pekee inayokubalika na Mwenyezi Mungu ni uislamu.
Uislamu ndio dini Mwenyezi Mungu anayoikubali kutoka kwa watumwa wake.
Mwenyezi Mungu ametuamrisha kuwa waislamu na kufuata sheria za kiislamu.
Uislamu ndio dini ya manabii wote. Manabii wote ni waislamu. Manabii wote wanamuamini Mwenyezi Mungu.
Nabii wa kwanza ni Sayidi wetu Adam, na wa mwisho ni Sayidi wetu Muhammad (Rehema ya Mwenyezi Mungu iwe juu yao)
Katika wakati wa Adam, watu walikuwa wakitamka, "La ilaha illallah Adam rasulullah."
Katika wakati wa Nuh, waislamu walikuwa wakitamka, "La ilaha illallah Nuh rasulullah."
Katika wakati wa Musa, waislamu walikuwa wakitamka, "La ilaha illallah Musa rasulullah."
Katika wakati wa Yesu, waislamu walikuwa wakitamka, "La ilaha illallah Issa rasulullah.'
Katika wakati wa Muhammad, waislamu wanatamka, "La ilaha illallah Muhammad rasulullah."
Mwenyezi Mungu anajua yote.
All Comments