Kenya imeongeza idadi ya wanajeshi wake katika maeneo ya mpaka wa Kenya na Somalia. Hali hiyo inafuatia hatua ya serikali kuimarisha usalama katika mpaka huo kufuatia tisho la wanamgambo wa al shabaab kutoka Somalia kutekeleza vitendo vya kigaidi. Katika kambi ya wakimbizi ya daadab, wasimamizi wanadai kuwa idadi ya wakimbizi 200 huwasili kila siku kutoka Somalia wanakokimbia vita vinavyoendelea kati ya wanajeshi wa serikali na wanamgambo hao.
Link to this comment:
All Comments (0)